Sema Naye
Headlines News :

NEWS

Latest Post

Diwani wa Chadema mbaroni

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Friday, October 11, 2013 | 9:59 AM



WATU tisa akiwemo Diwani wa Kata ya Old Moshi Magharibi, Elisaria Mosha (Chadema) wametiwa mbaroni wakituhumiwa kupokea fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia mradi wa umeme mkoani Kilimanjaro.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilal, kufanya ziara mkoani Kilimanjaro na kuagiza watu waliofanya hivyo wakamatwe mara moja.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema diwani huyo anatuhumiwa kujipatia Sh milioni 9.6 kwa njia ya udanganyifu.

Wengine wanaoshikiliwa ni Zakayo Kimathi (52) mkazi wa Mandaka, anayedaiwa kupokea Sh milioni 10.3, Oforo Kimambo (56) mkazi wa Mandaka anayedaiwa kupokea Sh milioni 29.

Wengine wanaotuhumiwa kupokea malipo hayo kwa njia ya udanganyifu ni Daud Mallya (69) mkazi wa Chekereni aliyepokea Sh milioni 8.6, Richard Mlaki (69) mkazi wa Kiboroloni alipokea Sh milioni 18.6 na Focus Herman (88) mkazi wa Kilototoni aliyepokea Sh milioni 36.

Boaz alisema kwa sasa watuhumiwa watatu hawajapatikana. Alieleza kuwa pamoja na watuhumiwa hao, polisi imemkamata Mwenyekiti wa Kijiji cha Mandaka Monono, Hassan Nduva (41) na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho, Vendelini Shayo (58) kwa kuhusika kufanikisha malipo hayo.

Dk Bilal alitoa agizo hilo mapema wiki hii wakati akizindua vituo vya kupozea na kusambaza umeme maeneo ya Kiyungi, YMCA na Makuyuni.

Alipokea taarifa kwa Mkuu wa Mkoa kuwapo kwa wananchi ambao hawakulipwa fidia zao, kutokana na kuwapo watu waliotumia ujanja wa kupokea fedha hizo, Sh milioni 169.2.

“Halmashauri ya Moshi Vijijini ndio ilikuwa wakala wa malipo hayo na ndio iliyofanya tathmini kwa kushirikiana na watendaji wa vijiji, ambapo wao walipeleka tathmini hiyo kwa Shirika la Umeme (Tanesco), ambalo lilitoa fedha hizo hivyo Tanesco hawahusiki,” alisema,” alisema Boaz.

Mwanademokrasia wa kweli hahitaji vurugu

http://www.nationsonline.org/maps/political_world_map3000.jpg

KATIKA jamii yeyote iliyostaarabika, kutofautiana kimawazo ni jambo lililo la afya katika maendeleo yake ;na ndio msingi wa kupata wazo bora na linaloweza kuboreshwa katika ushindani wa hoja.

Ni tofauti hizo za mawazo kwa wastaarabu, hujenga maslahi na vikundi maslahi katika jamii na hata katika mifumo ya siasa na vyama vya siasa duniani kote.

Ndio maana katika nchi yenye demokrasia, ikiwemo Tanzania, uongozi hauna budi kusikiliza sauti na mawazo mbadala, ili kupata wazo bora linalokubalika la lenye maslahi kwa wote.

Kwa hili, hatuna budi kuipongeza Serikali na hasa Rais Jakaya Kikwete binafsi kwa kuwa kiongozi mwanademokrasia, aliye tayari kusikiliza mawazo ya pande zote, hata kwa wanaomzushia.

Mwishoni mwa wiki iliyopita katika hotuba ya kila mwisho wa mwezi, Rais Kikwete aliendelea kuonesha alivyo mwanademokrasia wa kweli, pale alipowaambia Kambi ya Upinzani, kuwa maoni yao kuhusu Muswada wa Sheria ya Katiba, yanazungumzika.

Aliwaambia kwamba hata baadhi ya maoni hayo, yangeweza kukubalika kama wabunge wake wangekuwepo bungeni, ambako ndio chombo cha kuwasilisha mawazo mbadala na kujenga wazo bora.

Alisema bahati mbaya hawakuwepo, hivyo hapakuwepo mtu wa kusema mawazo yao na baada ya kupoteza fursa yao halali, kutaka kupata ufumbuzi nje ya Bunge ni jambo lisilowezekana. Alisisitiza kuwa masuala yanayohusu Bunge, hujadiliwa na kuamuliwa bungeni na si vinginevyo.

Pamoja na kambi hiyo iliyoundwa na NCCR-Mageuzi, CUF na Chadema, kupoteza fursa halali ya kutoa maoni yao bungeni, ambayo hutumiwa na nchi zote zilizokomaa kidemokrasia, Rais Kikwete amewapa fursa nyingine ya kukutana nao kati ya Jumapili ya Oktoba 13 mwaka huu, ama Jumanne ya Oktoba 15.

Uungwana huu wa Rais Kikwete kwa kweli ni wa kuungwa mkono, lakini pia unapaswa kuigwa na wanasiasa na vyama vyote vya siasa, kama kweli vinataka kushika dola na kuongoza taifa ambalo msingi na uimara wake ni umoja, mshikamano na undugu unaostawi katika jamii yenye utii wa sheria.

Tunasema hivyo kwa kuwa kila mmoja ni shahidi kuwa vyama hivyo havijakomaa kisiasa, kiasi cha kupewa dola, ambayo kuiongoza lazima watu wake wawe na umoja, mshikamano na udugu utakaostawishwa na uongozi unaoamini katika utii wa sheria.

Hakuna ambaye hakusikia viongozi hao, ambao baadhi yao wamewahi kuomba kura ili waongoze taifa hili, wakitamka hadharani kuwa watahamasisha Watanzania wasitii sheria na kubatiza Oktoba 10 mwaka huu kuwa siku ya kutotii sheria.

Tumejiuliza hivi kweli kiongozi anayetaka kuongoza taifa hili, kama ameiva na kukomaa kisiasa, anaweza kutangaza siku ya kutotii sheria?

Siku ambayo haina tofauti na kuhamisha watu kuvunja na kuiba mali za walipa kodi wanaowapa viongozi hao ruzuku kila mwezi kupitia vyama vyao?

Tumesikitika kuona viongozi hao wa vyama vinavyoungwa mkono na wananchi, wakihamasisha wananchi hao hao wasitii sheria, lakini tumefarijika, kusikia wamekubali busara za Rais Kikwete za kukaa meza moja na kumaliza tofauti zao.

Tunashauri kukitokea tofauti tena, ambazo tuna hakika zitatokea katika mambo mbalimbali tu kwa kuwa ndivyo jamii iliyostaarabika ilivyo, basi tuepuke kutoa kauli za namna hiyo, za kushawishi wananchi wasitii sheria, kwa kuwa ni kauli za jabu ambazo hakuna mwanademokrasia makini anayeweza kuziunga mkono.

Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria yaendelea na kazi zake Ofisi Ndogo za Bunge Dar

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Thursday, October 10, 2013 | 9:41 PM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEglm3OTjDA8dJOvScAZOwfjlvxZ6l2Si2bgdKwcN6jsGG-D162iRTVCXjH4QmxoqleGDZL6fF6eDP7S1lnAQMgYmAkjCsmOkp8QQVJPv51g7YTsrI1jbvFDP9BZ8uuerMgygV_jrK0L5a_o/s1600/A.JPG
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala Mhe. Pindi Chana (Mb) akifanua jambo mbele ya wajumbe wa kamati wakati wa kupitia muswada wa Sheria ya marekebisho ya Sheria Mbalimbali ( Miscellaneous Amendment Act 2013) wakati wa vikao vya kamati vinavyoendelea Ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2X175r4Cljjb1nRbS6rzQ8GhFZoB6pFYZaYvBcvtpNVb784k5cMOMYK8fTZGn_thxSqBtqaA3wtsOjkXUgCO4yO0CTIUGT0t25MxGcc5VXCvUVf_VbNvC14onl6siZx_46Lr_5oR-28sD/s1600/B.JPG
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala Mhe. William Ngereja (Mb) akijadili jambo na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Pindi Chana (Mb) wakati wa kikao cha kamati hiyo kujadili muswada wa Sheria ya marekebisho ya Sheria Mbalimbali ( Miscellaneous Amendment Act 2013) Ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam leo.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-HlkxJbpssVESprD08mxS9lVVHRfzBRyovn2wPREX1NZpv5OxlFF6cSwTgeXp7vr40QosdUmfTjALq1KSoNHvVAFo_ck9v-mf0E-QQQpecbHmgNp63BQkdl9ugTxajPuIia-Z0T40xH6U/s1600/E.JPG
Mhe. Tundu Lissu (Mb) ambaye pia ni mjumbe wa kamati hiyo akichangia jambo wakati wa kamati hiyo.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjuATq4yYH2mo12-Zpv2KOqslJSipFd1MLRBHYMBDlhlzzpOqVLeBgnGFDjkgSzjZwDLwmThAA04Dz2Sk6B9fsdsJH-6nPzhYCgiDixm1wHxHvbV5OPKlsxD1Gn9d7T25iB3q_iHkYsPbE3/s1600/F.JPG
Mhe. Mustapha Akunay (Mb) nae akichangia.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgmQxe0ow6p1hf8IfGSu8zX5Gw7olCLrby7rA7rmWIZdRpHIHqWYFjnS_-X7svdok8-QXDlJokl_a8EKPrv2tChbxJ_GFJBA1JQqd7pyWlgdxybbz5MtXuoyNBOk2M1DjQp5O6k_WPPYYMC/s1600/G.JPG
Mhe. Abbas Mtemvu.Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge

MKUTANO WA SITA WA VYAMA VILIVYOKUWA VYA UKOMBOZI KUZINI MWA AFRIKA WAFANYIKA DAR


 Katibu Mkuu wa sasa wa CCM, Abdulrahman Kinana, akisalimiana na Katibu Mkuu mstaafu Willson Mukama, walipokutana kwenye Mkutano wa sita wa Makatibu Wakuu wa vyama vilivyokuwa vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, leo katika hoteli ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wa NEC, Oganaizesheni CCM, Mohamed Seif Khatib
 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahmani Kinana akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Chama Cha FRELIMO cha Msumbiji, Philipe Paunde wakati wa mkutano huo
 
 Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro akishauriana jambo na Makatibu wenzake wa NEC, Zakia Meghji (Uchumi na Fedha) na Mohamed Seif Khatib (Oganaizesheni ) wakati wa mkutano huo. nyuma ni Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Sixtus Mapunda.
 
 Katibu Mkuu wa chama cha ZANU-PF cha Zimbabwe, Dydmus Mutasa akiwa kwenye mkutano huo.
 
Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Wilson Mukama akisalimiana na Dk. Asha-Rose Migiro wakati wa mkutano huo.
 
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa Chama Cha Kikomunisti cha Jamhuri ya Watu wa China, Ai Ping, wakati wa mkutano huo
 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Ai Ping wa chama cha CPC cha china wakati wa mkutano huo. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (zanzibar), Vuai Ali Vuai
 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwaelekeza jambo, Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wakati wa mkutano huo.
 
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza kabla ya kuanza kwa kikao hicho
 
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akifungua mkutano wa sita wa Makatibu wakuu wa vyama vilivyokuwa vya ukombozi kusini mwa Afrika, leo kwenye hoteli ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro na Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar, Vuai Ali Vuai.
 
Mkutano huo ukiendelea katika hoteli ya Kunduchi Beach

Mwenyekiti wa Mkutano wa Sita wa Vyama vilivyokuwa vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiendesha mkutano huo, leo katika hoteli ya Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Zanzibar Vuai Ali Vuai na kulia ni Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa CCM, Dk. Asha-Rose Migiro.
 
Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mkutano huo
 
 VIONGOZI wa vyama vilivyokuwa vya Ukombozi Kusini mwa Afrika, walioshiriki kwenye mkutano wa sita wa vyama hivyo, leo kwenye hoteli ua Kunduchi Beach, jijini Dar es Salaam, Kutoka kushoto, Katibu Mkuu wa Chama Cha ANC cha Afrika Kusini, Gwede Mantash, Katibu Mkuu wa chama cha ZANU-PF cha Zimbabwe, Didy Mutasa, Naibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Chana Cha Kikomunisti cha China, Ai Ping,Katibu Mkuu wa MPLA cha Angola, Julio Paulo. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa chama cha FRELIMO cha Msumbiji, Philipe Paunde na Katibu Mkuu wa Chama cha SWAPO cha Namibia,Nangolo Mbumba
 
Makatibu wakuu wa vyama vilivyokuwa vya ukombozi kusini mwa Afrika, wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine waandamizi, baada ya ufunguzi wa mkutano huo.
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha ZANU-PF, Didy Mutasa akionyesha alama ya hamasa ya chama chake, alipozungumza na waandishi wa habari, wakati wa mkutano wa makatibu wakuu wa vyama vilivyokuwa vya ukombozi mwa kusini mwa Afrika, kwenye hoteli ya Kunduchi Beach, Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM, Andulrahman Kinana na Wanne kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye.

UTEKELEZAJI WA AGIZO LA WAZIRI MAGUFULI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxcptv3FsGgQzBaVclFTlATy60R4fUakrCb6oss6QfVjJQJy_MHmgYHUm4Oir5QO9flyVmkVLSj95lcmGAVISCvkR-CvAhCgpRO_daDpq8w2uC7ngkKohj-1Wb-33hIZC4g5SzTut_VFj1/s1600/Picha+1.jpg
 Magari yakirekebisha uzito wa  mizigo baada ya kupimwa katika Kituo cha Mizani cha Mikese Mkoani Morogoro
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgDBcwn0sbY3HDGAFx0QxlB9RqSRRsJTToCQvfqxaJffC83rg6xbzuMXSGzD3ywdPRXwWQMU0_V-jFRmD5mmhtA3HJBIJ93uJsFb31nuhB5XXgjuapAJUcmWzxe6nXvtpwS1WoJeG5mM3VU/s1600/Picha+2.jpgMagari yakiendelea kupimwa katika Kituo cha Mizani cha Kibaha mkoani Pwani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEggFq-iNwwtIEX5hB04KtV-Wd_hqjsTH8HkIPq2d_3ftGaJ6LWC5JoDghl-dBnIAJw1hFAlxd7dbmrOj5YLIo8XzZZfV_ettqG9Evr9tEN_-ZjcTuYW6JtFA1cOoUWZwAh1ybXkYTu2Q30W/s1600/Picha+3.jpg Gari likiondoka baada ya kupimwa katika mzani wa barabarani likiwa limezingatia ya uzito uliowekwa kisheria.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEikHDE3pwXu3OFZbN7HD7eliMdWC3sk2xWa6SPMkmQkNYCq36Zyyx2LZGIJa1ecIFnsL9veC08hsN2j5NRiVvcs0yfifOYEiHj5IplMpGJ5RqSpMTEFaVhnlDFkx5ftdPzO7t9aAYdV1DO0/s1600/Picha+4.jpg Upimaji ukiendelea Kibaha
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjewOMgJJxo7pUKyad3RGdlRsomnpJQD-XCXJO4modgx5UzagepTnMKLNJy2fqUjj9VhtSpeL3F-aSFinxZdX8r5JC254-SP1IATsyjAD-F2M0cUPe6BtR0-RFR2ruHd308b8S_vm3S92-X/s1600/Picha+5.jpg Barabara ikiwa imebonyea kutokana na uharibifu unaotokana na magari yaliyozidisha uzito zaidi ya viwango vilivyowekwa kisheria..

JK azindua Shule ya Sekondari ya Miono, Bagamoyo

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg_awpBaYQqirujVbU7QiaLJkT9DExXJpZZO5fYVvc7ZF6eFT5tdrxJmieYTmdrlh4xoPtnJA0n67Fib9HqBkMib79Ya0OcJVh2ecg7b6or6aN1_JZ194LpfAxa9FdZNoCq3y-PhLFLch5u/s1600/D92A6377.jpg
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa katika jiwe la msingi kuizindua rasmi shule ya sekondari ya Miono iliyopo Wilayani Bagamoyo, akishuhudiwa na  Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mhe Philipo MulugoRais Kikwete yupo katika ziara ya kikazi Mkoa wa Pwani.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgPZxqMdiGvXFwzStao4h2kpaW5vwhIrQUnMtAQ9qDPxlidFVsbHTnyy5QmRZHpFFos0u59z-WMQViLSjst9TXPNCvweJ3VezmDEl5au1wBEzAwSbv-3yj9sVUsGrtcDaj2zyv2uj4LlhMK/s1600/D92A6347.jpg
 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikagua maktaba ya Shule ya Sekondari ya Miono Muda mfupi baada ya kuizindua shule hiyo jana Wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic3U7B_2IONJT23UHdZaOY7oWkDxa10uGhdTWDQgSNvBAfutjrSZrbrx3jzZpfUKfdVtIKu9LjCXtX9Y7ITZxTUq7FeIkBPDsh0z0QQq51l3_spF_W8byIAAaBZKCRjnix7VwMLcPqQlxj/s1600/D92A6311.jpg
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na  wanafunzi wa kidato cha tano wanaosoma Shule ya Sekondari ya Miono Wilayani Bagamoyo, Nyekwabi Jackline George,Penina Odara na Magret Machinyita wakitoa maelezo ya jaribio la sayani somo la biolojia wakati Rais alipofungua rasmi shule hiyo. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE MKOA WA MARA KWA MAFANIKIO MAKUBWA

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Wednesday, September 25, 2013 | 7:09 PM

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhIaGrYfY3q77_fkd80Fk0PbcU3ypkh-d-dTpDx7bXaongpN2lVpvCBS9Oi_jOlD7z9_Wu_T7a5Z1ZoFdERf1BZSCUdOcHPib1fCIxRzrBVKEyzNTxLozSUwLrPnHmLDd_3UpQS2gBTCbDI/s1600/1.jpg
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Musoma mjini kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Mkendo.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPSb9XD6BJdAnJq5A2BchcIb5uoG-bkavVad_a12jk052-HVQSqLsnUw3OvWbAZZmFk91LZO7LyU7jFvmL8SStVAwnK3TMbmXSg5vvhwQmD7A76sGi6TlxTgKWfGrOoeDDytIrKi3jLgUV/s1600/5.jpg
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Musoma mjini katika viwanja vya shule ya msingi Mkendo.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh8o2XoL6AOr5p9n7xyg1NlWM-4Yy3n5aV-bQSb7OZwupw9wu1gCRe9LhW6zFXCbz6lFVLAUsvVIo58uTVjw4VSadBamHrjOr1cLud08Q-GtRKDChx92r6SwsQuPTNBTPnDRoI_qvIgGJX2/s1600/19.jpg
Katibu Mkuu Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea zawadi ya sanamu ya mfano wake kutoka kwa Ndugu Elia Bugurilo Kamoga.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhElsLK74QqLSQfC4nPcyTboPgy_DM5IM4m5vyxguI9xwuXxD2S8CepMRZzZqM83fWyRLZ3GM4e21eQ7aUDU5eRay8KWDCKMwCJcNncFNVQsU8bBNS6334TXPEy8omCcw2BlIG4orocEV9X/s1600/16.jpg
Josephat Amon Muruga akiwa na wenzake sita baada ya kujiunga na CCM wakitokea Chadema.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjfqmojlgFLNAH4qBJ4gjh0XUBp7PdNBLFxVM5xIGFd2_XjlYSP76T-CPKQwJ5LBc4crOlu5g2kXbowKzV9tN_MWrLznEnt-KJ2Ty5SkDnj8kOyfql3A-X3RnM9UJUWOfP5aICie4D49oLm/s1600/12.jpg
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa anavuka na kivuko cha MV Musoma kutoka Kinesi kuelekea Musoma mjini,Kivuko hicho ambacho kimekuwa  mkombozi  wa usafiri kinauwezo wa kubeba abiria 330.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgRGLNTqduM3sPJFV06zdHOYceT9Hc4hSHJKLzB_YCwOIHO-pKxZrcBplKAPRmkIafXX_g0qTDYKPNzu0bal9QR2_KwE-QQpY5BC1rD3q-Y6GCqe_EM0ZyYGUMASN_SWNB8kep7kvmjleV_/s1600/13.jpg
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akijaribu vazi la kujiokoa wakati wa hatari wakati wa kuvuka  na kivuko cha MV Musoma.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgkLI8Ot4VoH5VKaVfhC1Uvj83XX2aKLNz3c4eKPugPw1i9kYsrzHx5K8AkoavsZbnDNwf9-e9c4xeW1UVltw5aYG092n3M8IOsKNjN5FR0XmTEiJ_R3r5W5T5DJIrFHG-nNU5s5tsGzqgg/s1600/7.jpg
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishangiliwa na Balozi wa shina namba 6 Tabitha Edgar wa kata ya Kitagi.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiH6vLtV5XrBon5YeAbgtl4jSQHnt3cYiDUTLWJ0G7LNJX6zJoCetGT6keqZUFkFpkmx-JLUZHiw_Vt-3db5-91AhLQzOJ1Q2peSPI_3vGmpTt9Fg28MlsdJWv1f8u8tgiALv5hckQfhEs8/s1600/8.jpg
Balozi wa nyumba kumi Tabitha Edgar wa shina namba 6 kata ya Kitagi akitoa shurani zake za kutembelewa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abbulrahman Kinana.
 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwArlombfD7pNj_mA5SF1vOdvVyBg_WTmSuu9RxfrqucnFo7hd4xxhZsOimUi5jzpF161jSeLgJsc-YNU81rMQcpYgj-Xfr5erEpsStZS1oGT22RnKb3EOD35VwLo-DpRQB3br8FVJW_33/s1600/10.jpg
Katibu Mkuu akipata maelezo ya ujenzi wa mradi wa maji kutoka ziwa Victoria uliopo eneo la Bukanga(Makoko) mradi huo utakamilika katikati ya mwaka ujao.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh8u2wyoWH_5xo1Ux1pZI0_HFlfwK5I3aOouakoLNxKzAdoZGi73l91zHk8iD9JCAxcJ142iyUdK_cjvuC5z9P7HbDPfdoj2N0XdvWkpuh6znHBGOyj4x0OkM0O7Mthu_wfvGPu7Olss86H/s1600/18.jpg
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akikagua maendeleo ya mradi mkubwa wa maji huku akipatiwa maelezo na mhandisi Jairos Chilema ,mradi huo utakuwa na bomba kubwa la kilomita tisini na ukikamilika utaondoa kabisa tatizo la maji Musoma Mjini.

CCM YAPOKELEWA KWA SHANGWE NA NDEREMO SHIRATU

KINANA AWEKA HISTORIA KATIKA VIWANJA VYA SHIRATI OBWERE MAELFU YA WATU WAFURIKA KUMSIKILIZA KATIBU MKUU VIONGOZI 43 KUTOKA UPINZANI WARUDISHA KADI WANACHAMA 126 WAJIUNGA HAPO HAPO

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiJo3zM2_opOo5IvKxpgCtFvBLeaOX9CPZWRq6yEeUmbRBzsnD-1FFmoKOGibgU50HFxwgmLSlPH5tufmJ488Gdt_Wdx7EpKdFePnQf46fD3zRSnvdQKNjsjpLMSc4NuN58BkQEWT3EXbB/s1600/gz1b.jpg
Mbunge wa Rorya Ndugu Lameck Okambo Airo akihutubia wakazi wa Shiratu waliofurika kwenye uwanja wa Shiratu Obwere,Mbunge huyo alieleza jinsi gani amefanikiwa kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSlcZDP1GEEbM3lgX55ZaVQ8Rl4gEKIfHev9Th8X4CiC3W8TnLe8G06cQB-TC7VaNsiBWH3cgaS2QuBqZmWDLSDh19d_lsFyhNtEOPukrVXEXf6rG8vCWB_vN4bBRVQIBHfUdBfMDnjEEJ/s1600/gz3b.jpg

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Ndugu Joseph Musukuma akiwasalimu wakazi wa Shiratu ,na kuwapongeza wananchi wa wilaya ya Rorya kwa umoja na mshikamano walio nao.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhSMXH7HPbLb4TDVvZpwI_3ntXJ5JARChn02WOPbIlO3a76KQ8hxzymjfdKTNKNXQ_UIY5_4KjjeyZlci0MGvxi4ufKpaMeHdTNNiQNHcTbK5I6ocVeWHBQV3BZ3UZojuXXT34LCbm-PBE0/s1600/gz4b.jpg

Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake nchini Ndugu Amina Makilagi akihutubia wakazi wa Shiratu kwenye mkutano wa hadhara ambao mgeni Rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgEWvHGV95cNDnwHBkEQNwgSrDkFQcuAuH_DYC41-54KF_gvX9ZRWk3d6VnNVohesdWj-vh6LFGWxnPqYh3Tq1l-WgIZcACnRPeNSFNgIAcMZgObFbrp_tGmLv1Wfs5bHZb8G8lxUxmrQAS/s1600/8.jpg
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Shiratu wilaya ya Rorya na kuwataka wananchi hao kuwapuuza wanaotaka kuharibu mchakato wa kupata Katiba Mpya kwani Mchakato wa Katiba hiyo imefuata taratibu zote za kisheria.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgDxzQjXdm0ZPLNSlOJAZHNExBg2F37Pn74ew1klHLlQeJZqHlpESTJgrHCqCjRZL91RQEeQTtjRrW90BWtipEt58dB7c95V2nOZ6GmkldZSvuQPzYfBqZoxLxHYiKGYLCrAmWxyMXPBgor/s1600/1.jpg

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Shiratu kwenye viwanja vya Shiratu Obwere na kuwaambia wakazi wa Shiratu kuwa CCM inatekeleza ahadi zake ilizoahidi kwa wakazi wa wilaya ya Rorya ,Katibu Mkuu aliwaeleza wananchi hao mipango iliyofanyika na itakayofanyika kwa ajili ya maendeleo ya wilaya hiyo,hasa katika suala zima la mradi wa umeme vijijini,maji,shule na huduma za afya.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVlfSejiHq1Vqwp5nriIomBn9sRpX43iZpHHVo0-yT5KE3A_la564fXM3YuG267U-MfL0hGCZKrotsc-eT-qq_uWiKfvVdK13o7PBhXI5TTXss7WARhvdJGJrH549ikkk0VfVu0WslD1mt/s1600/gzb11.jpg

Sehemu ya Umati wa watu walifurika kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye Uwanja wa Shiratu Obwere tarehe 24 Septemba 2013.

MAMA SALMA KIKWETE ATEMBELEA CHUO KIKUU CHA MONMOUTH HUKO NEW JERSEY-MAREKANI


 Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, Mama Salma Kikwete akipokewa rasmi na Dr. Paul Brown, Rais wa Chuo Kikuu cha Monmouth kilichoko huko New Jersey nchini Marekani mara tu baada ya kuwasili chuoni hapo tarehe 24.9.2013. Mama Salma yupo nchini Marekani akifuatana na Rais Jakaya Kikwete anayehudhuria Mkutano wa 68 wa Umoja wa Mataifa unaofanyika New York.

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa juu wa Chuo Kikuu cha Monmouth baada ya kuwasili chuoni hapo. Kulia kwa Mama ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein Mwinyi akifuatiwa na Naibu Balozi wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa Ramadhani Mwinyi, na Ms Janet Mahoney,wa Chuo Kikuu cha Monmouth na kushoto kwa Mama Salma ni Dr. Paul Brown, Rais wa Chuo Kikuu hicho, Bwana Saliba Sarsar, Makamu Rais wa Chuo cha Monmouth anayeshughulikia mahusiano ya kimataifa na Mwisho ni Bwana John McLaughlin, kutoka Shirika la Footprints for Education International la nchini Marekani.

 Rais wa Chuo Kikuu cha Monmouth Dr. Paul Brown,akimtembeza Mama Salma Kikwete maeneo mbalimbali ya chuo hicho. Kushoto ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein Mwinyi.

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongoza kikao cha pamoja kuhusu mashirikiano kati ya Taasisi ya WAMA na Chuo Kikuu cha Monmouth hasa katika masuala ya kuwaongezea uwezo wauguzi na wakunga. 
 
Mama Salma Kikwete aliongozana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein Mwinyi.

 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongoza kikao cha pamoja kuhusu mashirikiano kati ya Taasisi ya WAMA na Chuo Kikuu cha Monmouth hasa katika masuala ya kuwaongezea uwezo wauguzi na wakunga. 
 
Mama Salma Kikwete aliongozana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hussein Mwinyi.
 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea kikao cha pamoja kuhusu mashirikiano kati ya Taasisi ya WAMA na Chuo Kikuu cha Monmouth hasa katika masuala ya kuwaongezea uwezo wauguzi na wakunga. 

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea kitabu kutoka kwa Dkt. Edward Christensen, Vice President for Information Management. Chuo Kikuu hicho kilitoa zaidi ya vitabu  4000 kwa ajili ya Tanzania. Wengine wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni pamoja na Waziri wa Afya Dr. Hussein Mwinyi na Makamu Rais wa Chuo Bwana Sarsar na Mwishi ni nBwana John McLaughlin.
 
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anazungumza na Bwana Kevin Williams, Mwalimu kutoka shule ya Asbury Park. Shule hiyo ina uhusiano na shule ya sekondari ya WAMA, iliyoko huko Nakayama, wilayani Rufiji, mkoani Pwani. Katikati ni katibu wa WAMA Bw. Daudi Nasibu.
Picha zote na John Lukuwi


Na Anna Nkinda

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amekiomba chuo kikuu cha Monmouth cha mjini New Jersey nchini Marekani kufundisha wanafunzi wake lugha ya Kiswahili kama lugha ya kigeni ili wakazi wa eneo hilo waweze kuitumia katika mawasiliano pale itakapohitajika.

 Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) ametoa ombi hilo leo wakati akiongea na uongozi wa chuo hicho alipowatembelea yeye na ujumbe wake.

 Alisema hivi sasa lugha ya kiswahili inakuwa kwa kasi na kutumika katika maeneo mengi hasa nchi za Afrika Mashariki na Kati hivyo basi nao wawafundishe wanafunzi wao ili wakienda katika nchi hizo iwe ni rahisi kwao kuwasiliana.

 “Kiswahili ni lugha ya taifa letu la Tanzania ambayo tunaitumia katika mawasiliano, mkiwafundisha wanafunzi wenu lugha hii nao watawafundisha wenzao hivyo itakuwa ni rahisi kwao kuwasiliana hasa wakisafiri na kukutana na watu wanaotumia lugha hii”, alisema Mama Kikwete.

 Kwa upande wake makamu rais wa chuo hicho Dk. Edward Christensen alimshukuru mama Kikwete kwa kutembelea chuo hicho na kusema kuwa ombi lake la chuo hicho kufundisha lugha ya Kiswahili wamelisikia na wataangalia jinsi gani watalifanyia kazi.

 Aidha Dk. Christensen aliwaomba wakufunzi na watu wenye utaalamu wa mambo mbalimbali kutoka nchini Tanzania kwenda katika chuo hicho kufanya midahalo na wafanyakazi na wanafunzi wa chuo hicho.

 Chuo hicho kinawanafunzi wapatao 6300 kutoka ndani na n je ya nchi 29 na kinatoa kozi mbalimbali zikiwemo za Sayansi na sanaa katika ngazi ya cheti, shahada na shahada ya uzamili.





 
Support : 255-272-545-994 | Jasper A.K. | Mas Template
Copyright © 2011. Sema Naye - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger