Mwenge wa Uhuru wawasili Wilayani Masasi,Mkoani Mtwara - Sema Naye
Headlines News :
Home » » Mwenge wa Uhuru wawasili Wilayani Masasi,Mkoani Mtwara

Mwenge wa Uhuru wawasili Wilayani Masasi,Mkoani Mtwara

Written By Sema Naye - Naipenda Tanzania on Friday, September 20, 2013 | 10:39 AM


Mkuu wa wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Bi.Farida Mgomi akisoma taarifa ya wilaya baada ya kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru toka wilaya ya Newala makabidhiano yaliyofanyika katika Kijiji
cha Ndanda.


Msafara wa Mwenge ukikagua kitalu cha miti katika shule ya sekondari Ndanda.

Mdau Abdulaziz Video akitimiza wajibu wake.
 
Msanii nae akitoa burudani.
 
Picha na Abdulaziz Video,Masasi

Katika harakati za kuboresha kiwango cha Elimu wilayani Masasi Mkoani
Mtwara,Kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Juma Ali Simai amezindua
Chumba cha masomo ya komputa katika shule ya sekondari ya Ndanda
ambalo limegharimu kiasi cha shilingi milioni 49 zilizotolewa na
wahisani mbalimbali ikiwemo mamlaka ya mawasiliano nchini(TCRA).

Uzinduzi huo uliofanyika katika mbio hizo utawezesha wanafunzi kupata
elimu ya kompyuta na tehama ili kuwajengea uwezo wanafunzi hao
kutokana na upungufu mkubwa wa Vitabu kufuatia kompyuta hizo kufungwa
pamoja na huduma ya Intanet.

Akizungumza wakati akizindua jengo hilo la komputa Juma Simai
aliwataka wanafunzi kutumia kompyuta hizo kwa ajili ya kujifunza
zaidi ili kupata elimu juu ya masomo na si kwa kuangalia mambo ambayo
hayatasaidia katika maisha yao ikiwemo utandawazi unaoendelea Duniani
ikiwa pamoja na mambo ambayo hayafuati maadili ya Elimu.

Awali akipokea Mwenge wa Uhuru toka wilaya ya Newala,Mkuu wa wilaya ya
Masasi,Bi Farida Mgomi alibainisha kuwa pamoja na wilaya hiyo
kukimbiza Mwenge huo kwa kilometa 120. 

Miradi itakayotembelewa na kuzinduliwa kabla ya kuukabidhi katika wilaya ya Nanyumbu.
Kwa upande wao baadhi ya wanafunzi walioongea na globu hii walieleza
kuwa uzinduzi wa Chumba cha komputa utasaidia kwa kiasi kikubwa
kuboresha elimu yao.

Mwenge ukiwa wilayani Masasi umetembelea, jumla ya miradi 10 kati ya
miradi hiyo imefunguliwa,kuwekewa mawe ya msingi na kutembelewa yote
ikiwa na thamani ya shilingi Bilioni 2.4 ikiwemo chumba cha kompyuta
kwenye shule ya sekondari ya Ndanda,mradi wa umwagiliaji maji wa
Mpowora,upandaji wa miti ya mbao katika kijij Mwenge i cha Mwen
nda,ujenzi wa mahabara ya kisasa kwenye kituo cha afya cha Chiwale na
kutembelea vikundi vya wajasilia mali,

Pamoja na shamra hizo za mwenge pia kulipambwa na burdani ya 
Bendi ya Vijana Jazz ya Dar es sallam
Share this article :

0 comments:

 
Support : 255-272-545-994 | Jasper A.K. | Mas Template
Copyright © 2011. Sema Naye - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger