
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akishiriki kwa vitendo kufyatua matofali na vijana wa CCM walioweka kambi katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika Mji mdogo wa laela tarehe 22 Septemba 2013. Lengo kuu la kambi hiyo ni kuwajenga vijana katika itikadi na sera za Chama cha Mapinduzi, Ukakamau na Uzalendo kwa chama na nchi yao kwa ujumla. Katika kambi hiyo wanajishughulisha pia na kazi za kijamii kama kufyatua matofali zaidi ya 6,000 yatakayosaidia katika kujenga kituo cha afya Laela. Katika kuwapa nguvu kuendeleza kambi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alitoa mchango wa laki mbili taslim.




(Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.)
0 comments:
Post a Comment